Saturday, 11 March 2017

IJUE KWELI YA MUNGU KUHUSU UFALME WA MUNGU ,KANISA LA MUNGU .


 Ninakusalimu katika jina la BWANA WETU YESU KRISTO ALIYE HAI.

Nakukaribisha katika blog hii ambapo utapata kujifunza mengi kuhusu UFALME WA MUNGU,WOKOVU na mengine mengi ya kimasisha.

SOMO:  KANISA LA MUNGU NA HUDUMA ZAKE( JIFUNZE KUHUSU KANISA)

  

A:KANISA LA BWANA YESU KRISTO.
     I.        Maana ya Kanisa.
   II.        Aina za kanisa .
 III.        Chanzo cha kanisa la Agano jipya.
 IV.        Mifano ya kanisa.
   V.        Kazi (HUDUMA ZA KANISA).
 VI.        Nafasi ya ROHO MTAKATIFU katika Kanisa.                                                                                                                                                              VII.        Hitimisho .

1.    MAANA YA KANISA
Maana isiyo ya Kibiblia.
·         Jengo la kanisa mara nyingi watu huita KANISA.-katika agano la kale majengo haya yalitwa;SINAGOGI,HEKALU.
·         Dhehebu au kundi la watu katika dini ya Kikristo.

  Maana ya “KANISA” katika Agano la kale
v  Neno  KANISA ni asili yake limetokana na nene la kiyunani linaloitwa   EKKLESIA
v   Neno –EK likiwa na maana ya “KUTOKA KWA”
v  Neno – KLESIA lina maana ya “KUITWA”
v  Neno  EKKLESIA” likiwa na maana ya –KUITWA KUTOKA KWA.
v  HIVYO neno
 KANISA katika Agano la kale lilimaanisha ;watu ambao wameitwa kutoka kwenye DHAMBI na dunia na ambao wamekusnyika kwa lengo moja.
Maana ya KANISA katika Agano jipya
ü  Waumini wa kwanza katika Agano jipya, walitumia neno kanisa kumaanisha ifuatvyo;


ü  MKUSANYIKO WA WAAMINI NA WAUMINI katika IMANI YA KRISTO.
ü  WARUMI 16:4-15; NISALIMIENI NA KANISA LILILOMO KATIKA NYUMBA YAO.
ü  WAGALATIA 1:2, 1THESALONIKE 1:1.

ü  Ni kundi lote la watu waliozaliwa mara ya pili( UMOJA WA WAKRISTO ULIMWENGUNI KOTE) 1PETRO 1:23. Yakobo 1:18,
ü  Watu walionunuliwa kwa damu ya YESU KRISTO. MATENDO YAMITUME 20:28. UFUNUO 14:4-5.

2.    AINA ZA KANISA
                                                     I.        JENGO
                                                   II.        WATU WA MAHALI PAMOJA
                                                 III.        MTU BINAFSI(MIMI NA WEWE)

3.    CHANZO CHA KANISA LA AGANO JIPYA.
v  MSINGI WA KANISA hili NI YESU KRISTO , BWANA NA MWOKOZI WETU.
v  Kanisa sio shirika la kibinadamu ,kama wengine walivyolifanya.
v  MATHAYO 16:18, “NA JUU YA MWAMBA HUU NITALIJENGA KANISA LANGU;WALA MILANGO YA KUZIMU HAITALISHINDA
v  WAEFESO 2:20-22.
v  KANISA LA KRISTO lilizaliwa SIKU YA PENTEKOSTE,ambayo Ahadi ya BABA ya ROHO MTAKATIFU ,ilitimia na MITUME WAKAJAZWA ROHO MTAKATIFU
v  MATENDO 2:1-4, MATENDO 2:41. Watu elfu tatu walipata wokovu siku hiyo, na KANISA likaanzia hapo.

WASHIRIKA  WA KANISA
a)    Mtu anakuwa mshirika wa KANISA la KRISTO mara tu baada ya KUOKOLEWA (MATENDO 2:27)
b)    Watu wengi wamekuwa washirika wa madhehebu mbalimbali ya dini,,bila kuwa WASHIRIKA WA KANISA LA KRISTO.
c)    MTU anapokuwa MKRISTO anahitaji kuungana NA WAUMINI wa KANISA la BWANA ili KUIMARISHA kanisa LA MUNGU.
d)    WASHIRIKI WA KANISA LA KWELI
ü  NI WATAKATIFU-Tumetenganishwa na maisha ya dhambi na tunamwishia MUNGU. WARUMI 1:7
ü  NI NDUGU. WARUMI 8:29
ü  NI WAAMINI.
ü  NI WATEULE.

4.    MIFANO YA KANISA
                                     I.        KANISA NI BIBI –ARUSI NA MWANAKONDOO
v  UFUNUO 21:2
“Nami nikauona mji ule mtakatifu,Yerusalemu  mpya,ukishuka kutoka mbinguni kwa MUNGU,umewekwa tayari,kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe
v  UFUNUO 21:9, MATHAYO 25:6,, YOHANA 3:29. UFUNUO 19:7.
v  BWANA –ARUSI NI YESU KRISTO, KANISA LINAPASWA KUJENGA MSINGI WAKE katika UTAKATIFU.

                                  II.        MASKANI YA MUNGU (HEKALU LA BABA,MWANA NA ROHO MTAKATIFU)
·         YOHANA 14:23    “YESU akajibu,akamwambia,Mtu akinipenda,atalishika neno langu; na BABA  yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya MAKAO kwake
·         YOHANA 14:16-17    “ Nami nitamwomba BABA, naye atawapa Msaidizi mwingine,ili AKAE nanyi hata milele” “bali ninyi mnamtambua ,maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu”
·         1WAKORINTO 6:19-20    AU hamjui ya kuwa mwili wenu ni HEKALU LA ROHO MTAKATIFU aliye ndani yenu,mliyepewa na MUNGU? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; Maana  mlinunuliwa kwa THAMANI. Sasa basi,mtukuzeni MUNGU katika miili yenu.
·         UFUNUO 21:3, 1KORINTO 3:16, 2KORINTO 6:16.
·         KILA mshirika wa KANISA la KRISTO ATAMBUE uthamani huu MKUU tuliopewa na MUNGU,,ili TUWEZE KUKAA katika hali YA UTAKATIFU.

                                III.        MWILI WA KRISTO YESU,MWOKOZI.
Ø  1WAKORINTO 12:24-37.  27  BASI NINYI MMEKUWA MWILI WA KRISTO,NA VIUNGO KILA KIMOJA PEKE YAKE”
Ø  YESU NDIYE BWANA na KIONGOZI MKUU wa kanisa.
Ø  KILA MUUMINI,ni mshirika wa MWILI HUU.
Ø  Wauumini wanahitaji kushirikiana ili waweze kuishi katika MWILI wa KRISTO.
Ø  KILA mwamini ni Mtu na kiungo MUHIMU cha KANISA. Hata kama kinadharauliwa na kuonekana ni cha kawiada bado NI CHA MUHIMU SANA.
Ø  KILA mshirika katika MWILI huu lazima awe na uhusiano wa moja kwa moja na MKUU WA KANISA –YESU KRISTO.
Ø  KANISA NI MWILI WA KIROHO WA YESU kujidhihirisha kwa ULIMWENGU.
Ø  Hivyo washirika,  wote  tunapaswa kuhimizana,kusaidiana na kufanya kazi kwa pamoja ili kuujenga mwili wa KRISTO.
Ø  WAEFESO 4:16  Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila KIUNGO,kwa kadri ya utendaji wa kila sehemu moja kwa moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika UPENDO

                                 IV.        KANISA NI NGUZO NA MSINGI WA KWELI
1TIMOTHEO 3:15
NI mahali ambapo watu hufundishwa kweli yote ya NENO LA MUNGU.

                                   V.        KANISA NI CHOMBO MILIKIWA NA MUNGU MWENYEWE
TITO 2:14. ,  1 PETRO 2:9
ü  NYUMBA YA ROHO
ü  UKUHANI MTAKATIFU
ü  MAWE YALIYO HAI
ü  MZAO MTEULE
ü  UKUHANI WA KIFALME
ü  TAIFA TAKATIFU
ü  WATU WA MILIKI YA MUNGU.
ü  TAIFA LA MUNGU.

5.    KAZI (HUDUMA YA KANISA LA KRSTO)
MUNGU ,BWANA YESU KRISTO aliweka na kuanzisha KANISA ili kuleta UTUKUFU WA JINA LAKE.
v  Kazi hizi tunaweza kuziangalia katika sehmu tatu ambazo zinamtukuza MUNGU
                                                     i.        KWA NJE’ > INJILI YA YESU KRISTO
                                                    ii.        KWA NDANI’ > TUNAPOJENGANA SISI KWA SISI
                                                  iii.        ‘KWA JUU’ >KATIKA IBADA


KAZI ZA KANISA
A.     Kuhubiri injili kwa  kila kiumbe ulimwenguni kote( HABARI NJEMA ZA UFALME WAMUNGU)
MARKO 16:15, MATHAYO 28:19-20.   1PETRO 2:9,MATENDO 1:8.
B.   Kujengana Nafsi (mwili wa KRISTO)  1KORINTO 14:26.
C.   HUMFANYIA MUNGU IBADA . WEABRANIA 13:15, 10:25.  NJIA ambazo tunamwabudu MUNGU
v  Kukusanyika pamoja, mathayo 18:20,,ebrania 10:25.
v  Kupitia mziki na nyimbo. Waefeso 5:19,, zaburi 50:23,ZABURI 150
v  Kwa njia ya MAOMBI        .MATENDO 2:46-47,4:24. MARKO 11:17
v  KUTOA
v  Kwa NJIA YA ROHO MTAKATIFU
v  KUHIDHABIHU NMIILI YETU, WARUMI 12:1-2.
D.KANISA HUMRUSU ROHO MTAKATIFU katika HUDUMA ZOTE. 1KORINTO 12:4
E.HUFUNDISHA KWELI YA NENO LA MUNGU.kupitia vipindi mbalimbali,Sunday school,vijana.
F.HUBATIZA KWA MAJI MENGI. MATHAYO 28:19
G.HUKUMBUKA KIFO CHA BWANA kwa njia ya MEZA YA BWANA. LUKA 22:20.
H. HUFANYA USHIRIKA MBALIMBALI, kuomba kwa pamoja, kula kwa pamoja na kushirikiana.
I.kanisa HUSHEREKEA, mfano;ndoa,watoto kuombewa,vifo, Christmas,pasaka,siku  ya BWANA
J.KANISA HUKUA
K.HUHUDUMIA WATU; KUSAIDIA wahitaji,waliopotea,na kuwalea waumini wapya.
PIA kazi nyingine muhimu ni pamoja na
v  KUMTII KRISTO kwa kuwatii wnadamu. WAEBRANIA 13:17, TITO 3:1-2. 1THESALONIKE 5:12, MALAKI 2:7.
v  KUITEGEMEZA NYUMBA YA MUNGU
v  KUIJENGA NYUMBA YA KUABUDIA
v  KUITEGEMEZA NYUMBA YA MCHUNGAJI
v  1WAKORINTO 9:7-11; MATHAYO 25;31-46;
v  KUTOA ZAKA   MALAKI 3:10-12., MITHALI 10:27. MITHALI 3:9-10.


6.    NAFASI YA ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA LA LEO. ROHO wa MUNGU ndio chanzo cha KANISA LA KWANZA ,hivyo basi tunapaswa kutambua na kumpa nafasi ya PEKEE na ya  KWANZA katika MAISHA YETU na HUDUMA katiKA kanisa lake.
ü  Wagalatia 4:6, waefeso 4:4
ü  YEYE ndiye kiongozi,mwalimu wetu  hivyo ni vyema katika maamuzi yote tuyafanyayo KUMSHRIKISHA ili tuweze kukua KATIKA IMANI YA YESU KRISTO.
ü  KANISA ,tunapaswa kusisitiza kila mmoja wetu, kuhusu KUJAZWA NA kutembea,kuishi katika ROHO MTAKATIFU

7.    HITIMISHO
“KANISA ni MWILI HALISI WA KIROHO WA YESU KRISTO, hivyo tunapaswa kuwa na kutmbea na kuishi katika UTAKATIFU
v  LUKA 18: 7-8  NA MUNGU,JE! HATAWAPATIA HAKI WATEULE WAKE WANAOMLILIA MCHANA NA USIKU, NAYE NI MVUMILIVU KWAO?8 NAWAAMBIA,ATAWAPATIA HAKI UPESI; WALAKINI, ATAKAPOKUJA MWANA WA ADAMU, JE!ATAIONA IMANI DUNIANI?
HESHIMA NA UTUKUFU KWAKO BWANA NA MWOKOZI WETU YESU KRISTO UNAYE TUWEZESHA! Barikiwa sana wote.By jbrev.







     

No comments:

Post a Comment