Wednesday, 26 July 2017

SHARING THE GOSPEL (KWA NINI INJILI YA YESU KRISTO INAHUBIRIWA).

Hellow wana wa Mungu, ninakukaribisha katika blog hii ambayo utapata mafundisho mbalimbali kuhusu ufalame wa Mungu na maisha yako. Karibuni sana na BARAKA NA NEEMA ZITOKAZO KWA MUNGU ZIWE PAMOJA NAWE! 

SOMO: KWA NINI INJILI YA YESU KRISTO INAHUBIRIWA DUNIANI? (sharing the Good news). 

MATHAYO 28: 18-20. "Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi, na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siki zote, hata ukamilifu wa dahari.

MARKO 16:15-20.  LUKA 24:46-49,YOHANA 20:19-23, Matendo ya mitume 1:8. Ni maneno ya mwisho ya Bwana Yesu kabla ya kurudi kwa Baba Mbinguni, anaagiza Wanafunzi wake kwa Habari ya kupeleka Habari za Ufalme wa Mungu Ulimwenguni Kote. NI AMRI KWA KILA MWAMINI KATIKA IMANI YA YESU KRISTO. 

A:MAANA YA UINJILISTI ni kuzungumza, kupeleka, kumwambia mtu au watu habari njema za UFALME WA MUNGU. (good news or The Gospel of Jesus Christ).

MATHAYO 3: 2 "TUBUNI KWA MAANA UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA" Ni sauti ya Yohana Mbatizaji.

MATHAYO 4:17 "Tokea wakati huo YESU alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni ;kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia"  Ni sauti ya Yesu Kristo. 

MATENDO YA MITUME 2: 38 "Petro akawambia, Tubuni mkbatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu"  Ni sauti ya petro.

MATENDO 17:30 "Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni ; bali sasa anawaagiza watu wote  wa kila mahali WATUBU"  Ni sauti ya paulo. 

🎤 Kiini cha Maneno yote na Biblia Ni UKOMBOZI WA MWANADAMU. Watu wanaitaji kusikia Habari za Msamaha wa dhambi ambao Mungu Baba ametoa kupitia njia ya kumwamini Yesu Kristo..

B: KWA NINI HABARI NJEMA ILIKUWA LAZIMA( why is the "Good News" necessary?

  1. MUNGU, ambaye ni mwenye Haki na Mtakatifu, alituumba KWA MFANO NA SURA YAKE (MWANZO 1:26-28). Mungu Baba kupitia Yesu Kristo anatafuta kurudisha Sura yake katika Utukufu wake.                                                                                                               LUKA 19:10 "KWA KUWA MWANA WA ADAMU ALIKUJA KUTAFUTA NA KUOKOA KILE KILICHOPOTEA"      Watu wote ni sura ya Mungu, wanahitaji kuokolewa.                       TOKA mbinguni Mungu anatazama sura yake, Hataki iendelee kuwa chini ya Utumwa wa giza na shetani. 
  2. Mwanadamu wa kwanza Adamu, alianguka katika DHAMBI na kuwa nje ya Ushirika pamoja na Mungu,  hivyo akaipoteza SURA YA MUNGU aliyoumbwa kwayo. (MWANZO 3:1-21)  Mwanzo 3:9 "BWANA MUNGU AKAMWITA ADAMU, AKAMWAMBIA UKO WAPI? ni sauti ya Mungu inasikika baada ya mwanadamu kutenda uasi.  
  3. Wanadamu wote tu wazao wa Adamu, hivyo baada ya Adamu,  wanadamu wote tumezaliwa katika sura ya Adamu, kila anayezaliwa anazaliwa katika dhambi.                MWANZO 5:3 "Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa SURA YAKE, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi.  Hivyo hakuna aliye salama, WATU WOTE TUNAMWITAJI YESU, WAKUBWA KWA WADOGO!   Injili ni lazima. 
  4. Mwanadamu amekuwa nje ya Mungu kwa mda mrefu sana, hivyo mwanadamu ametumikia giza na kufikia hatua ya  kupenda giza kuliko NURU.                         (YOHANA 3:19) "Na hii ndyo hukumu;ya kuwa Nuru imekuja ulimwenguni,  na watu wakapenda giza kuliko nuru;kwa maana matendo yao yalikuwa maovu"  (TUNAHITAJI KUHUBIRI HABARI ZA YESU AMBAYE NI NURU ILI KILA MTU AJUE HABARI HIZI) 
  5. Hakuna njia nyingine zaidi kwa mwanadamu mtenda dhambi na muasi kuweza kuwa na mahusiano na MUNGU  MTAKATIFU NA MWENYE HAKI.   Njia pekee ni kupeleka Habari Njema za TOBA NA MSAMAHA WA MUNGU, kwa sababu ni TOBA YA KWELI kwa njia ya DAMU YA YESU ambayo hutupatanisha Kwa Mungu na kurudisha USHIRIKA WETU PAMOJA NA MUNGU BABA. 
C:HALI YA MWANADAMU NJE YA YESU KRISTO! (NJE YA NEEMA YA WOKOVU
  • Watu wote ni wenye dhambi na wako chini ya Hukumu ya Kifo.                               Warumi 5:12" Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi ilingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti;na hivuo mauti ikawafakianwatu wote kwa sababu watu wote wamefanya dhambi"    WARUMI 3:21 "Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu"  waebrania 9:27.

  • Watu wote wanahesbiwa kuwa wamekufa kwa sababu ya makosa na dhambi.   WAEFESO 2:1 "Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu" Dhambi husababisha Kifo cha kiroho, kuondoka kwa Roho mtakatifu na kifo cha kimwili. 
  • Watu wote ni watoto wa Hasira  na huenenda kwa tamaa za kimwili. WAEFESO 2:3.

  • Watu wote wamefarakana na kuwa mbali na uzima wa MUNGU. WAEFESO 4:17-18..

  • Watu wote wema, waungwana na wenye kutenda mema WANAITAJI KUOKOLEWA. Warumi 3:23,Wote wamefanya dhambi, YOHANA 3:3 "YESU AKAJIBU, AKAMWAMBIA, AMIN, AMINI, NAKUAMBIA, MTI ASIPOZALIWA MARA YA PULA, HAWEZI KUUOONA UFALME WAA MUNGU"

  • Watu wote wasio mpokea Yesu na kurudi katika mahusiano mazuri na Mungu, WAMEWEKEWA HUKUMU YA MILELE AMBAYO NI UHARIBIFU NA ADHABU KATIKA JEHANAMU YA MOTO. (UFUNUO 20:10-15). 
🎤HIVYO, INJILI INAHITAJIKA KWA HARAKA SANA KWA WATU WOTE, ILI KULITIMIZA KUSUDI  LA MUNGU  AMBAYE ANATAMNI WATU  WOTE WAOKOLEWE... LET US GO, GO, GO AND PREACH THE GOOO NEWS OF SALVATION. 

D: HABARI NJEMA NI NII(Wahat is the "Good News) 

âž•Mungu aliamua kumrudisha mwanadamu tena katika Mahusiano yake KWA KUMTUMA YESU KRISTO KUWA MWOKOZI WA ULIMWENGU (Mwanzo 3:26-29),YOHANA 3:16, YOHANA 1:12. Hivyo Mwanadamu amepewa nafasi nyingine katika Ufalme wa Mungu, Ya kuwa Mwana wa Mungu na Raia wa ufalme wa Mungu. Mtu anapomwamini Bwana Yesu  anafanyika MWANA KATIKA UFALME WA MBINGUNI. 

1.Yesu pia ni sura ya Mungu (Waebrania 1:3).
2.Yesu hakutenda Dhambi kama Adamu. (Waebarnia 4:15)
3.Yesu amebeba na kuchukua Dhambi zetu. 

 WARUMI 5:8 "BALI MUNGU AONYESHA PENDO LAKE YEBMWENYWE KWETU SISI, KWA KUWA KRISTO ALIKUFA KWA AJILI YETU, TULIPOKUWA TUNGALI WENYE DAHMBI" 

➕WOTE WANAOMPOKEA KRSTO KAMA MWOKOZI, WANAKUBALI KAZI ILIYOMALIZIKA PALE CALVARY MSALABAINI kama NJIANPEKEE YA WOKOVU, wanatubu dhambi zao na Kukiri Kuws Yesu ni Bwana na wanazliwa katika Krsto na kufanyika WATOTAO WA MUNGU. Yohana 3:1-5.
YOHANA 14:6 "YESU AKAMWAMBI, MIMI NDIMI NJIA, NA KWELI NA UZIMA;MTU HAJI KWA BABA, ILA KWA NJIA YA MIMI"

1.Tunahesabiwa kuwa na HAKI kwa njia ya KUMWAMINI YESU TU. (Warumi 4:5,22-25)
2.HAKUNA HUKUMU KWA WALIO KATIKA YESU. WARUMI 8:1-2.
3.TUNAPATA TENA SURABYA MUNGU KWA NJIA YA YESU KRISTO(Tunakuwa Raia wa mbinguni TENA) Waebrania 8:28-30.
4.TUNAPATA AMANI KATIKA KRISTO YESU. (WARUMI 5:1)"Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. "
5.TUNAPATA UHURU WA KWENDA KWA BABA MUNGU kwa njia ya Yesu Kristo.                       WARUMI 5:2.

âž•Mwanadamu anarudishwa katika USHIRIKA KAMILI WA BABA NA KUWA WASHIRIKA WA  UTUKUFU WA UTAJIRI WA MUNGU. (Ephesia 1:18,Wakolosai1:27,Roma 9:23).

âž•MUNGU AMETOA NJIA MOJA YA WOKOVU KWA WANADAMU WOTE, wayahudi na wa mataifa. (warumi 3:10,5:21.) NI YESU KRISTO PEKEE AMETOLEWA NA  MUNGU KUWA MWOKOZI WA ULIMWENGU. 

E: NANI MWENYE JUKUMU LA KUHUBIRI HABARI NJEMA KWA ULIMWENGU?? 

  1. KANISA LA KRISTO, kuanzia Mwamini mmoja na watu wote. Mathayo 16:18,1petro 1:12.MUNGUhufanya kazi yake kupitia watu wake. 
  2. Ujumbe wa INJILI LAZIMA UHUBIRIWE KUPITIA SAUTI ZA WATU WA MUNGU(WARUMI 10:13-15)
  3. KANISA au WAAMINI NI LAZIMA KUUFIKIA ULIMWENGUna watu wote Kabla ya KURUDIBKWA YESU MARABYA PILI, kwa sababu baada ya hapo HAKUNA NAFASI NYINGINE. (2Wathesalonike 4:13-18)
  4. KANISA lisipofanya kazi ya INJILI YA YESU, haitaweza kufanyika. (Waefeso 3:8-12).HIVYO NI MUHIMU KANISA TUONDOKE NA KUHUBIRI HABARI HIZI NJEMA KWA WATU WA MUNGU. 
🎤MATHATO 24:14 "TENA HABARI NJEMA YA UFALME ITAHUBIRIWA KATIKA ULIMWENGU WOTE, KUWABUSHUHUDA KWA MATAIFA YOTE, HAPO NDIPO MWISHO UTAKAPOKUJA" 
Imetupasa kuhubiri.. Habari hizi.. Ambazo ni TOBA NA MSAMAHA WA DHAMBI KWA WANADAMU KWA NJIA YA YESU KRISTO. 

F: NI MAANA YA KUWA MSHUHUDIAJI WA HABARI NJEMA? ( TO BE A WITNESS) 
  1. Kuwa tayari kutoa ushuhuda wa yale uliyoona na kushudia na kusikia. 1Yohana 1:1-4.
  2. Kuishi maisha yanayoedena na Ukiri wako WA WOKOVU.  Maisha ya kumfuata Bwana Yesu Kristo. 1Wakorinto 11:1.
  3. Kuishi maisha ya NURU kupitia KUTENDA MATENDO MEMA kwa wati na kwa Mungu pia (KUMPENDEZA MUNGU NA WANADAMU PIA),  Saidia watu, zungumza  kama Mwana wa Mungu,  Be Honest. 
  4. Ni kuzungumza na kushirikisha habari njema kwa watu popote, nafasi inapofungiwa. LUKA 21:13.

G:VITU MUHIMU KATIKA HUDUMA HII VYA KUFAHAMU! NA KUZINGATIA. 

  1. YESU YUPO PAMOJA NASI SIKU ZOTE.   Muhimu ni sisi KUKAA NDANI YAKE. MATHAYO 28:20b, "NA TAZAMA, MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE, HATA UKAMILIFU WA DAHARI"                                                                                              YOHANA 15:5 "Mimi ni mzabibu;ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana;MAANA PASIPO MIMI NINYI HAMWEZI KUFANYA NENO LOLOTE" 
  2. ROHO MTAKATIFU NI MTU MUHIMU SANA KATIKA KAZI HII YA INJILI. Hivyo tunamwitaji  ROHO MTAKATIFU, kwa ajili ya  kutupa NGUVU YA KUPELEKA INJILI KILA MAHALI... Naye YUPO PAMOJA NASI MILELE.    MATENDO YA MITUME 1:8 "Lakini mtapokea nguvu,  akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashaidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote,  na samaria,  na hata mwisho wa nchi"
  3. KUWA NA IMANI KATIKA MUNGU, YESU NA ROHO MTAKATIFI, Tukijua ya kuwa anayeokoa  na kutenda ni MUNGU.                                                                             YOHANA 14:12 "Amini, amin, nawambia, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam na kubwa kulikobhizo atafanya,  kwankuwa miki naenda kwa Baba. 
  4. KUHUBIRI NA KUZUNGUMZA KUSUDI LA MUNGU(Ni muhimu sana kujua na kuyazungimza Mapenzi ya Mungu kwa watu wake na si matakwa yetu)   MATENDO YA MITUME 20:27 "KWA SABABU SIKUJEEPUSHA NA KUWAHUBIRIA HABARI YA KUSUDI LOTE LA MUNGU"   Ni muhimu sana, tuhubiri KIINI KIKUBWA CHA KUJA KWA YESU AMBACHO NI WOKOVU WA MWANADU! 
  5. YOTE YAFANYIKAYO,  UTUKUFU WOTE TUNAMPA MUNGU AMBAYE NDIYE ANAYEOKOA, ANAPONYA, ANATENDA MAAJABU. Sisi ni watumishi wake tu, na imetupasa kufanya hivyo.                 .            .  .... .                                                        
  6. FAHAMU KUWA MUNGU KIU YAKE NA MOYO WAKE ATAKA WATU WOTE WAOKOLEWE. 

🎤1TIMETHEO 2:1-6,  3 "HILO NI ZURI, NALO LAKUBALIKA MBELE ZA MUNGU MWOKOZI WETU, AMABAYE HUTAKA WATU WOTE WAOKOLEWE, NA KUPATA KUJUA YALIYO KWELI"  KWA SABABU MUNGU NI MMOJA, NA MPATANISHI KATI YA MUNGU NA WANADAMU NI MMOJA, MWANADAMU KRISTO YESU"

Ubariwe sana kwa kufuatilia somo hili,  unaweza kufuatilia masomo. Mengine pia kupitia blog hii. 

Be blessed. JESUS LOVES YOU SO MUCH THAT HE DIED ON THE CROSS FOR US!! LET US GO, GO, GO AND SPEAK GOOD NEWS TO ALL PEOLE. 
Jemrath bikombo. Jbrev@0753775948.


Monday, 24 July 2017

UWAKILI WA MUNGU (STERWARDSHIP OF GOD)


  • Hellow watu wa MUNGU, nakukaribisha katika blog hii ambayo unapata masomo mbalimbali kuhusu UFALME WA MUNGU na Maisha yako. Ubarikiwe sana. Karibuni sana.


SOMO :UWAKILI WA MUNGU.  SISI NA VITU VYOTE NI MALI YA BWANA.

Mwanzo 1:1 " HAPO MWANZO MUNGU ALIZIUMBA MBINGU NA NCHI"   MUNGU ndiye mmiliki wa kila kitu, aliyeumba, NDIYE ANAYEMILIKI VITU VYOTE!
ZABURI 24 :1 "NCHI NA VYOTE VIIJAZAVYO NI MALI YA BWANA, DUNIA NA WOTE WAKAAO NDANI YAKE" 


A. MAANA YA WAKILI : Ni mtu aliyepewa dhamana juu ya mali ya mtu mwingine! 

KUMBUKA, katika kitabu cha MWANZO 1:28-31. Mungu MUUMBA alitukabidhi mali yake ili tuitunze kwa UTUKUFU wake.
WAKILI (manager, steward, administrator).


  • UWAKILI unaonyesha mahusiaano makubwa kati ya Mungu na Mwanadamu.  "GOD as a OWNER and Man as a MANAGER"

MUNGU ametuweka sisi kuvisimamia vitu vyote tulivyo navyo katika maisha yetu. (it is a DIVINE TRUST).

SIFA KUU ZA MAWAKILI AMBAO MUNGU ANATAFUTA. 
1.MAWAKILI WAAMINIFU.
2.MAWAKILI WENYE BUSARA.

  • WAKILI MWAMINIFU ni yule anayetambua kwamba yeye na vitu alivyonavyo ni MALI YA MUNGU. Pia huishi na kutumia vyote kwa ajili ya MUNGU. 

  • WAKILI Mwenye BUSARA huilinda mali ya BWANA wake na kuendelea kuzalisha na kuzaa matunda mpaka BWANA wake ATAKAPOKUJA, hakati tamaa, NI mvumilivu. Anawajibika kwa mali ya BWANA wake. (LUKA 12:42-48). 

MATHAYO 25 :14 - 30. (WATUMISHI waliopewa TALANTA).


  1. HAGAI 2:8 "Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu, ASEMA BWANA wa MAJESHI. 
  2. ACTS 17 :25" Kwa maana ndiye anayewapa wote uzima na Pumzi yangu, ASEMA BWANA "
SISI sio wamiliki wa maisha yetu na vitu vyetu, MUNGU ametuweka kuwa MAWAKILI WAKE. 1WAKORINTO 4:1-2" Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa KRISTO na MAWAKILI wa siri za MUNGU. Hapo tena inayohitajiwa katika MAWAKILI, ndiyo Mtu aonekane kuwa MWAMINIFU "

N.B :WAKILI MWEMA anafanya mambo yote kwa faida na HESHIMA na UTUKUFU WA BWANA WAKE.

B:MAENEO YETU YA UWAKILI, AMBAYO MUNGU AMETUPA!

  1. UWAKILI WA MUDA WETU. Muda ni  kitu cha muhimu Sana, kwa sababu muda ukipita umepita, haujirudii tena. Tunapaswa kutumia mda wetu vizuri kwa UTUKUFU wa MUNGU.                                                                                                                                  Pia tunahitaji kutumia muda wetu vizuri kwa ajili ya HUDUMA, KAZI, FAMILIA., Masomo.  1PETRO 4:2.    , 1 korinto 10:31.                                                                Waefeso 5:15-16 "MKIUKOMBOA WAKATI KWA MAANA ZAMANI HIZI NI ZA UOVU".
Tusitumie mda huu mchache tuliopewa na MUNGU duniani kufanya yasiyo mpendeza, bali TAFUTA KUYAFANYA MAPENZI YA MUNGU kila mda, Pangilia mda wako na TUMIA MDA HUU KUYAANDAA MAISHA YAKO YA MILELE. Baada Ya mda huu hatutapata mda . Mwingine. 
     2. UWAKILI WA MIILI YETU. 

  • Tumeumbwa kwa sura na mfano wa MUNGU. 
  • Mungu anaagiza tuitoe miili yetu iwe dhabihu na kuifanya ibada. 
  • Tunapaswa kumpenda MUNGU kupitia miili yetu.  WARUMI 12:1. 
  • Miili yetu ni mahekalu ya ROHO MTAKATIFU. 1 korinto 3:16 " au hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hakalu la ROHO MTAKATIFU na ya kuwa Roho wa anakaa ndani yenu?. 
  • Kuishi maisha matakatifu na kujitenga na dunia na kumkaribia MUNGU. 
  • Hatupaswi kuitumia miili yetu kwa dhambi na uovu.   
  • Pia MUNGU anatamani tuitunze miili yetu na afya zetu,, kula vizuri, PUMZIKA, fanya mazoezi. 
  • Tuishi kwa ajili ya MUNGU tu 1.Kumuabudu 2.Kumtii 3.Kuwa HAI katika Bwana na kufa kwa habari ya dhambi. 
          3.UWAKILI WA MALI ZETU. 
"KUTOKA 19 :5 "Maana dunia yote ni mali yangu"   Tukumbuke kwamba ndiye  anaayetupa mali na vitu vyote tulivyo navyo. Tunapaswa kuvitumia kueneza UFALME WAKE

AYUBU 41 :11 "Ni nani aliyetangulia kunipa hata nimlipe? Kila kilicho chini ya mbingu nzima ni CHANGU" 
MUNGU anaagiza tutumie mali tulizopewa kwa ajili ya UTUKUFU wake, mfano, Nyumba, gari, Ardhi. 

         4.UWAKILI WA KARAMA, VIPAWA, TAALUMA NA HUDUMA
MFANO, Uimbaji, karama za ROHONI, Udaktari, Ualimu, komputya, ufundi umeme, na kila Kazi yoyote unayofanya. 
Vyote hivyo, MUNGU amekupa kwa ajili ya kutumika Kuujenga UFALME WAKE UNAVITAWALA.. WAEFESO 4:11 - 16. 

5.UWAKILI WA FEDHA ZETU NA UTAJIRI
Mungu ametupa fedha kwa ajili ya UTUKUFU wake na kueneza Kazi yake. KURUDI la Mungu kuhusu Fedha ni kuwabariki Watoto wake, kutuwezesha Kuishi maisha yenye BARAKA KWA kujifunza KUTOA NA KUPOKEA!

KWA NINI TUTOE FEDHA ZETU.

  1. BIBLIA TAKATIFU INATUFUNDISHA UTOAJI (malaki 3:8-12) 
  2. NI AGIZO LA YESU (LUKA 6:8) 
  3. TUNAONYESHA UPENDO WETU KWA MUNGU (1 korinto 13 :4)
  4. TUNAWEKA HAZINA KWA MUNGU. 
  5. NI HERI KUTOA KULIKO KUPOKEA Acts 20:35). 
  6. KRISTO mwenyewe ALIJITOA kama sadaka kwa ajili yetu. 
  7. KWA AJILI YA KUENEZA UFALME WA MUNGU NA KAZI YA MUNGU DUNIANI. 
  8. Tunapaswa kumtolea MUNGU kwa HIARI, FURAHA, UTIIFU, UHURU, UWIANO, UKARIMU NA KWA DHABIHU. 
  9. Tukumbuke kumtolea MUNGU ZAKA (FUNGU LA KUMI) MWANZO 14 :18-20) SADAKA inayonyesha kwamba MUNGU NDIYE ANAYEMILIKI. 
    C: FOUR PRINCIPLES OF STEWARDSHIP!

THE FUNDAMENTAL PRINCIPLE OF ALL PEOPLE States that " we own nothing, God owns everything, we are simply managers "

1.THE PRINCIPLE OF OWNERSHIP (UMILIKI) Genesis 1:1,ZABURI 24. God created everything, He only owns everything.

2.THE PRINCIPLE OF RESPONSIBILITY (UWAJIBIKAJI). Mungu ana HAKI ya UMILIKI, MAWAKILI wana wajibika. Mungu ametuita kusimamia MALI yake,Tunapaswa kuwajibika.

3.THE PRINCIPLE OF ACCOUNTABILITY. (KUTOA HESABU)   WARUMI 14 :12 "Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za MUNGU"
Tutatoa HESABU ya vile tilivyokabidhiwa (Time, money, ability, information, wisdom, authority, talents, work Education, relationship, resources and opportunities).

4.THE PRINCIPLE OF REWARD ( MALIPO).  
MATHAYO 25 :21 "BWANA wake akamwambia, vema, mtumwa mwema na MWAMINIFU, ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya Mengi, ingia katika FURAHA YA BWANA wako"
Wakolosai 3:23 - 24.

MUHIMU SANA :"There is no greater choice offered to us than surrender to the one who CREATED us and knows us better than we know ourselves "

SWALI LA KUKUMBUKA :LUKA 18 :8  " WALAKINI, ATAKAPOKUJA MWANA WA ADAMU, JE, ATAIONA IMANI DUNIANI?

ubarikiwe sana kwa kujifunza. UTUKUFU KWA MWOKOZI YESU KRISTO ANAYEOKOA NA KUTUPA ROHO MTAKATIFU KUTOKA KWA MUNGU BABA. Amen.

Jemrath Bikombo.